Marekani ime eleza baraza la usalama la umoja wa mataifa kuwa Washington ita jibu madai ya shambulizi la silaha ya kemikali dhidi ya mji unao shikiliwa na waasi nchini Syria, bila kujali kama Umoja wa mataifa utachukua hatua au la.
Ila Urusi ume onya Marekani kuhusu matokeo mabaya yatakayo jiri, iwapo Marekani itafanya shambulizi dhidi ya serikali ya Syria.
Staffan de Mistura ndiye mjumbe maalum wa umoja wa mataifa, ame omba baraza la usalama lifanyie madai ya shambulizi hilo uchunguzi wa kina.
Tangu mgogoro huo ulipo anza nchini Syria mwaka wa 2011, umoja wa mataifa umekadiria zaidi ya watu wapatao 470,000 wame uawa, na mamilioni yawa Syria wame kimbilia sehemu tofauti nchini humo na ng’ambo kwa sababu ya mgogoro huo.
Share






