Vikao vya bunge la shirikisho vime anza tena baada ya likizo ya mwezi mzima, kwa kiongozi wa upinzani Peter Dutton na waziri mkuu wa zamani Scott Morrison kuzungumzia shutma zilizo tolewa wakati wa likizo kuhusu mienendo yao ya awali.
Serikali ya Labor inatarajiwa pia kuwasilisha muswada wayo wa nyumba, ambao umekwama ndani ya seneti na pia itawasilisha muswada wakuongeza malipo ya Jobseeker.
Mawaziri wa zamani wa chama cha Liberal wamejibu shtuma za makosa dhidi yao walipokuwa mamlakani, muda mfupi baada ya vikao vya bunge kuanza baada ya likizo ya wiki tano.
Share






