Mada kadhaa zimejadiliwa katika kongamano la 35 la Umoja wa Afrika, moja kati yao ikiwa ni ombi la bara la Afrika lipewe nafasi yakudumu katika baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Ma bara ya Afrika, na Amerika Kusini ndiyo tu ambayo hayana uwakilishi wakudumu katika baraza la usalama la umoja wa mataifa. Bara la Asia nilawakilishwa na China, wawakilishi wa Ulaya wakiwa: Ufaransa, Uingereza na Urusi na mwanachama wa tano wakudumu katika baraza la usalama ni Marekani.
Kongamano hilo lili jadili pia mbinu zaku kabili usambaaji wa maambukizi ya virusi vya UVIKO-19, upatikanaji wa chanjo za UVIKO-19 pamoja na migogoro inayo endelea kuzikabili baadhi ya nchi barani Afrika, wenyeji wa kongamano hilo Ethiopia wakiwemo katika orodha hiyo.
Ungana na mwandishi wetu Jason Nyakundi kwa taarifa hii.
Share






