Wafanyakazi wa umma kuongezewa mshahara NSW

Bronnie Taylor, waziri wa afya ya kanda NSW.

Bronnie Taylor, waziri wa afya ya kanda NSW. Source: AAP

Wafanyakazi wa sekta ya umma jimboni New South Wales, wanatarajia nyongeza ya asilimia tatu kwa mishahara yao.


Wakati huo huo serikali ya jimbo hilo ina inua kikomo cha malipo ya mwaka huu baada ya miezi ya hatua za viwanda.

Kiongozi wa jimbo hilo ametangaza pia uwekezaji wa bilioni 4.5 za dola, kwa mfumo wa afya ambao unakabiliwa na matatizo, sehemu ya msaada unao tolewa unajumuisha mpango waku waajiri wafanyakazi wa matibabu elfu kumi, pamoja na kutoa dola elfu tatu za ziada kwa wafanyakazi walioko katika mfumo wa afya kwa saa.

Serikali ya jimbo ina inua pia kikomo cha malipo kwa sekta ya umma, ambayo imekuwa ikitumia tangu 2011. Malipo yanatarajiwa kuongezeka kutoka 2.5% hadi 3% katika mwaka huu wa fedha. Malipo hayo yataongezeka tena hadi 3.5% mwaka ujao yakitegemea uzalishaji wa waajiriwa. Hiyo ni hatua inayo wathiri wafanyakazi laki nne wa serikali jimboni wanao jumuisha wafanyakazi wa afya, walimu, maafisa wa jeshi la polisi na wanao fanya kazi za usafi.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service