Wanamgambo wa kundi la ADF wenye uhusiano na kundi la Islamic State waliua wanafunzi 41 na kuteka nyara wengine sita katika shambulio kwenye shule kaskazini mwa Uganda karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, jeshi lilisema Jumamosi.
Wanajeshi walipata miili ya waliokufa walipofika shuleni, msemaji wa jeshi Felix Kulayigye alisema katika taarifa.
Kulayigye alisema mapema Jumamosi kwenye Twitter “Jeshi lilikuwa linamsaka adui ili kuwaokoa waliotekwa nyara na kuangamiza kundi hilo.”
Maafisa wa polisi na jeshi wanasema washambuliaji walikua watano na walitia moto bweni baada ya kupora chakula na vitu vingine .
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.






