Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Waziri Gwajima:"Tanzania haina mpango wakupokea chanjo ya COVID-19"

Dkt Dorothy Gwajima Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Tanzania

Dkt Dorothy Gwajima Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Tanzania Source: Ikulu Tanzania

Wizara ya Afya nchini Tanzania imesema Jumatatu haina mpango wa kupokea chanjo ya COVID-19 ambayo imekuwa ikiripotiwa kuwepo na kutumika katika mataifa mengine.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Doroth Gwajima amesema : ““Wizara ya Afya haina mpango wa kupokea chanjo ya Covid 19 inayoripotiwa kuwepo na kutumika katika mataifa mengine, ifahamike kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya inayo taratibu za kufuata pale inapotaka kupokea bidhaa yoyote ya afya baada ya Serikali kujiridhisha hivyo kwa nia njema kabisa ni hadi tujiridhishe na si vinginevyo.”

Nako nchini Uganda, mwanasiasa Robert Kyagulanyi anayejulikana pia kwa jina lausanii Bobi Wine, amefikisha hoja mahakamani kuomba matokeo ya uchaguzi mkuu yafutwe, na uchaguzi mpya uandaliwe kwa sababu ya madai ya wizi wa kura.

Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now