Aliyekuwa waziri wa afya wa Rwanda, Dkt. Diane Gashumba amejiuzulu.
Kujiuzulu kwa Dkt. Diane Gashumba, kulithibitishwa na afisi ya waziri mkuu nchini humo.
Katika ujumbe uliochapishwa kwenye mtandao wa Twitter, afisi hiyo imesema kwamba kujiuzulu kwake kunatokana na makosa ya kawaida na mapungufu yake ya uongozi. Hatahivyo haikutoa maelezo zaidi kuhusu sababu zilizomlazimu kujiuzulu.
Kujiuzulu kwake kunajiri wiki moja tu baada ya mawaziri wengine wawili kutangaza kujiuzulu.
Share





