Wiki ya tatu ya kampeni ya uchaguzi mkuu yatawaliwa na gharama ya maisha

Kiongozi wa Upinzani wa shirikisho Anthony Albanese, arejea katika kampeni ya uchaguzi mkuu.

Kiongozi wa Upinzani wa shirikisho Anthony Albanese, arejea katika kampeni ya uchaguzi mkuu. Source: SMH POOL

Wiki ya tatu ya kampeni ya uchaguzi mkuu ili tawaliwa na shinikizo za gharama za maisha, baada ya mfumuko wa bei kuongezeka kwa 5.1%.


Kiongozi wa chama cha Labor Anthony Albanese, alirejea katika harakati za kampeni baada ya wiki nzima yakujitenga baada yakupatwa na UVIKO-19. Wakati huo huo viongozi wawili wa vyama vikubwa nchini wame endelea kujadili lini watafanya mjadala mwingine wakitaifa. Mivutano katika ukanda wa Pasifiki nayo, ime endelea kuongezeka kuhusu jinsi Australia ilivyo simamia mkataba wa usalama.

Wiki ijayo itajumuisha mijadala kadhaa kuhusu sera kati yamawaziri na mawaziri kivuli, na kuna uwezekano kutakuwa mjadala mwingine kati ya Scott Morrison na Anthony Albanese. Ila mjadala kuhusu uwezekano wa mijadala, umezuia tarehe ya mjadala kuamuliwa. Waziri Mkuu amekubali kufanya mjadala kupitia vyombo vya habari kama Channels 7 na 9, ila Bw Albanese anapendekeza mjadala ufanywe katika kikao chakitaifa cha waandishi wa habari.

Bw Albanese alifanya vizuri zaidi katika mjadala wa kwanza wiki jana dhidi ya waziri mkuu hata hivyo, mjadala wa pili itabidi ufanywe haraka zaidi kabla ya siku ya uchaguzi mkuu itakayo kuwa katika wiki 3 zijazo.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Wiki ya tatu ya kampeni ya uchaguzi mkuu yatawaliwa na gharama ya maisha | SBS Swahili