Albanese aunga mkono ongezeko ya mshahara kwa wafanyakazi wa pato la chini

TONY BURKE MINIMUM WAGE PRESSER

Australian Employment Minister Tony Burke speaks to the media during a press conference at Parliament House in Canberra, Friday, March 31, 2023. (AAP Image/Lukas Coch) NO ARCHIVING Source: AAP / LUKAS COCH/AAPIMAGE

Serikali ya shirikisho imependekeza wafanyakazi wenye pato la chini nchini Australia, waongezewe mshahara ila, serikali haija sisitiza kuwa ongezeko hilo la mshahara liwe sambamba na mfumuko wa bei.


Serikali imeunga mkono nyongeza ya mshahara kwa wafanyakazi nchini wenye pato la chini, ikitoa uwasilishaji wayo kwa mapitio ya mwaka wa mishahara ya Tume ya kazi, kabla ya uamuzi wayo Juni.

Uwasilishaji wa serikali hauja toa pendekezo la kiwango cha nyongeza ya mshahara ila, ime hamasisha tume hiyo “ihakikishe mishahara halisi yawa Australia wenye pato la chini hairejei nyuma".

Hata hivyo, haija dokeza pia kuwa “mishahara yote inastahili ongezeka kulingana na mfumuko wa bei ", au kuwa mfumuko wa bei ndiyo sababu pekee ambayo Tume ya Haki kazini inastahili zingatia.

Chama kinacho wakilisha wafanyakazi A-C-T-U, kwa upande wacho kina weka shinikizo kwa ongezeko la kima cha chini cha mshahara wa 7%, pamoja na mishahara mingine kulingana na mfumuko wa bei.

Wakati Chumba cha Biashara na viwanda nchini Australia, kimependekeza ongezeko la kima cha chini cha 3.5% au 75c kwa saa, hadi $841.04 kwa wiki.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Albanese aunga mkono ongezeko ya mshahara kwa wafanyakazi wa pato la chini | SBS Swahili