Burundi imejipata katika sintofahamu yakikatiba baada ya Rais Peter Nkurunziza, kufariki ghafla tarehe 8 Juni 2020.
Rais Nkurunziza alikuwa anatarajiwa kumkabidhi mamlaka Rais mteule Evariste Ndayishimiye tarehe 20 Agosti kabla yakustaafu rasmi.
Kifo chake cha ghafla kimewaacha wanasiasa na raia wa Burundi, ndani na nje ya nchi hiyo, wakiwa namaswali yasiyokuwa na majibu.
Mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya SBS mjini Bujumbura Ramadhani Kibuga, alituarifu hatua ambazo zimechukuliwa na wanasheria kutatua kitendawili hicho.
Share





