Usiku wa kuamkia tarehe 24 Julai 2020, Rais wa Jamahuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kwa masikitiko makubwa, aliutangazia umma kutokea kwa kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa.
Kufuatia kifo hicho, Tanzania ilitangaza siku saba za maombolezo na kutumia Uwanja wa Mpira kwa siku tatu kuwapa wananchi wote, fursa ya kuaga mwili wa kiongozi huyo aliyezikwa siku ya Jumatano wiki hii Mkoani Mtwara.
Mtayarishaji wetu wa vipindi FRANK MTAO, aliungana na baadhi ya wafuatiliaji wa mambo ya siasa kuchambua kwa ufupi ungwe ya uongozi wa Marehemu Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa.
Share





