Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE starting June 12 2026

Taarifa ya habari 10 Julai 2025

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Kiongozi wa Tasmania wa chama cha Liberal anatarajiwa kuitisha rasmi uchaguzi wa mapema hii leo, hatua itakayo rejesha jimbo hilo la kisiwa katika uchaguzi wa pili katika muda wa miaka mbili.


Published

Updated

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Kiongozi wa Tasmania wa chama cha Liberal anatarajiwa kuitisha rasmi uchaguzi wa mapema hii leo, hatua itakayo rejesha jimbo hilo la kisiwa katika uchaguzi wa pili katika muda wa miaka mbili.


Kundi la wazima moto wa Australia, wana elekea nchini Canada kuwasaidia washirika wao ambao wanakabiliana na moto wa nyika jimboni Alberta. Maafisa hao wanatumwa chini ya masharti ya mkataba wa makubaliano yaliyo anzishwa kati ya nchi hizi mbili, zinazo husiana na ushirikiano ambao unaweza hitajika katika matukio ya dharura.

Mgogoro kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Rwanda umechukua sura mpya kufuatia uamuzi wa Rwanda kujitoa katika Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika ya Kati (ECCAS). Rwanda inadai kuwa DRC ilishirikiana na baadhi ya nchi wanachama wa ECCAS kuizuia kuchukua nafasi ya uenyekiti wa jumuiya hiyo.

Idara ya Polisi nchini Kenya inamulikwa kwa kifo cha kutatanisha cha Mwalimu Albert Ojwang', aliyekuwa maarufu kwenye mitandao ya kijamii. Ojwang' alifia kwenye korokoro ya kituo kikuu cha polisi jijini Nairobi baada ya kukamatwa kwao katika jimbo la Homa bay kwa madai ya kuchapisha taarifa za uwongo kwenye mtandao wa X.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now