Taarifa ya habari 10 Julai 2025

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Kiongozi wa Tasmania wa chama cha Liberal anatarajiwa kuitisha rasmi uchaguzi wa mapema hii leo, hatua itakayo rejesha jimbo hilo la kisiwa katika uchaguzi wa pili katika muda wa miaka mbili.


Kundi la wazima moto wa Australia, wana elekea nchini Canada kuwasaidia washirika wao ambao wanakabiliana na moto wa nyika jimboni Alberta. Maafisa hao wanatumwa chini ya masharti ya mkataba wa makubaliano yaliyo anzishwa kati ya nchi hizi mbili, zinazo husiana na ushirikiano ambao unaweza hitajika katika matukio ya dharura.

Mgogoro kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Rwanda umechukua sura mpya kufuatia uamuzi wa Rwanda kujitoa katika Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika ya Kati (ECCAS). Rwanda inadai kuwa DRC ilishirikiana na baadhi ya nchi wanachama wa ECCAS kuizuia kuchukua nafasi ya uenyekiti wa jumuiya hiyo.

Idara ya Polisi nchini Kenya inamulikwa kwa kifo cha kutatanisha cha Mwalimu Albert Ojwang', aliyekuwa maarufu kwenye mitandao ya kijamii. Ojwang' alifia kwenye korokoro ya kituo kikuu cha polisi jijini Nairobi baada ya kukamatwa kwao katika jimbo la Homa bay kwa madai ya kuchapisha taarifa za uwongo kwenye mtandao wa X.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service