Taarifa ya Habari 14 Machi 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Mawaziri wa ngazi ya juu katika serikali yamadola, waongeza juhudi kutuliza wasiwasi kandani kuhusu Australia kupata manowari zinazo tumia nguvu ya nyuklia.


Chama cha Liberal cha NSW kime lazimishwa kumtema mmoja wa wagombea wao chini ya wiki mbili kabla ya uchaguzi wa NSW, wakati mgombea mwingine amejipata hatarini kwa madai aliyotoa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa. Mgombea wa chama cha Liberal wa eneo bunge la Wyong ambalo liko katika kanda ya Central Coast, alivuliwa ugombea wa chama kwa sababu ya machapisho yakukera katika mtandao wa jamii ambayo yalijumuisha madai yakukera kuhusu wapenzi wa jinsia moja, Uislamu na chanjo.

Utafiti wamajaribio kutoka chuo cha Griffith cha Queensland, umepata viungo kati ya madhara ya Uviko wa muda mrefu na ugonjwa wa uchovu sugu kwenye ubongo.

Makamu wa Rais Kamala Harris atafanya ziara ya wiki moja barani Afrika mwishoni mwa Machi huku Marekani ikiongeza mawasiliano yake kwa bara hilo huku kukiwa na ushindani wa kimataifa, haswa na China. Bi Harris atafanya ziara Ghana kuanzia Machi 26 hadi 29, kisha Tanzania kuanzia Machi 29 hadi 31. Na kituo chake cha mwisho kitakuwa Zambia Machi 31 na Aprili mosi.

Watu wapatao 11 wamekufa katika mji wa Blantyre, Malawi na wengine 16 hawajulikani walipo baada ya kimbunga Freddy kuikumba nchi hiyo mwishoni mwa juma. Msemaji wa polisi ya Malawi, Peter Kalaya ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba timu ya uokozi inawatafuta watu katika vitongoji vya Chilobwe na Ndirande, ambavyo vimeathiriwa vibaya.





Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 14 Machi 2023 | SBS Swahili