Taarifa ya Habari 16 Juni 2025

Bench - Swahili.jpg

Waziri Mkuu Anthony Albanese, amesema mazungumzo kati yake na mshiriki wake kutoka Canada katika mkutano wa G7, ilikuwa fursa yaku imarisha tena uhusiano kati ya nchi hizo mbili.


Rais wa Marekani Donald Trump amesema serikali yake haija husika katika mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran siku ya Ijumaa 13 Juni. Mwana diplomasia mkuu wa Iran Abbas Araghchi, amesema Iran ina ushahidi thabiti kuwa vikosi vya Marekani vili isaidia Israel katika mashambulizi yake.

Udhibiti wa sekta ya malezi ya watoto uta imarishwa, na hatua za lazima zita anza kutekelezwa kuanzia Septemba mosi. Mageuzi hayo yame afikiwa na mawaziri wa elimu kutoka majimbo na wilaya zote za Australia.

Walimu katika Kaunti ya Kisumu wameapa kugoma kuanzia Jumatatu wakitaka Naibu Mkuu wa Polisi, Eliud Lagat, ajiuzulu kufuatia kifo cha mwalimu na mwanablogu Albert Ojwang’.

Ulinzi ume endelea kuimarishwa katika kanisa la Askofu Gwajima, hatua ambayo ime walazimishwa waumini kufanyia ibada barabarani.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service