Taarifa ya Habari 20 Mei 2025

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Jimbo la Victoria lina tarajia kupata ziada yake ya kwanza tangu janga la UVIKO-19, wakati serikali ya Allan itakapo toa bajeti ya jimbo hii leo Jumanne 20 Mei 2025.


Moja ya kampuni kubwa ya nishati nchini Australia, ime waomba wateja wake msamaha, ikisema kukabiliana na kaboni haizuii au kuondoa madhara yanayo sababishwa na kuchoma mafuta. EnergyAustralia ilitoa taarifa Jumatatu 19 Mei 2025, kufuatia kesi iliyo funguliwa na Parents for Climate ambayo ilikuwa imeratibiwa kusikizwa ndani ya mahakama ya shirikisho ya New South Wales wiki jana.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewaonya wanaharakati ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki kuingia Tanzania na kutoa matamko yanayoweza kuchochea uvunjifu wa amani katika taifa hilo. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa sera ya mambo ya nje, toleo la mwaka 2024, Rais Samia Suluhu Hassan ametumia jukwaa hilo kuwaonya wanaharakati ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki kuacha kuingia nchini na kutoa matamko yanayoweza kuvuruga amani ya nchi.

Utawala wa Rais William Ruto umetishia kumtia mbaroni aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua kwa kuchochea ghasia, hatua ambayo ikichuliwa itazidisha uhasama kati ya viongozi hao wawili waliofanya kazi pamoja na kutwaa uongozi wa nchi 2022. Wikendi, Naibu Rais Profesa Kithure Kindiki na Waziri wa Usalama wa Ndani Kipchumba Murkomen walimwonya Bw Gachagua, wakisema anapandisha joto la kisiasa kutimiza ajenda yake ya kisiasa kuelekea uchaguzi wa 2027.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service