Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE starting June 12 2026

Taarifa ya Habari 22 Mei 2025

Bench - Swahili.jpg

Kiongozi wa New South Wales, Chris Minns, amesema rasilimali za ziada zinatolewa kwa jumuiya ambazo zime athiriwa kwa mafuriko, katika eneo la kati ya pwaZaidi ya idadi ya watu elfu 48,000 kwa sasa wame tengwa kwa sababu ya maji ya mafuriko.


Published

Updated

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS


Share this with family and friends


Kiongozi wa New South Wales, Chris Minns, amesema rasilimali za ziada zinatolewa kwa jumuiya ambazo zime athiriwa kwa mafuriko, katika eneo la kati ya pwaZaidi ya idadi ya watu elfu 48,000 kwa sasa wame tengwa kwa sababu ya maji ya mafuriko.


Vitu kumi na moja muhimu vya kitamaduni, vinarejeshwa katika maeneo yao ya asili nchini Australia, baada ya takriban karne moja ng’ambo. Vioo kumi vya vichwa vya mikuki na, jino la la kangaroo vime kuwa karibia miaka 100 ndani ya nyumba ya makumbusho ya Fowler mjini California.

Serikali ya Kenya kupitia Waziri wake wa Mambo ya Nje, Musalia Mudavadi imethibitisha kuwa bado mwanaharakati Boniface Mwangi anashikiliwa na mamlaka za Tanzania na kwamba juhudi za kumrejesha Kenya zinafanyika. Wanaharakati hawa walishikiliwa na polisi mei 19 wakiwa hapa nchini ambako walifika kwa ajili ya kufuatilia mwenendo wa kesi ya uhaini inayomkabili, Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, CHADEMA, Tundu Lissu.

Ange Postecoglou amesema ushindi wa timu yake katika fainali ya kombe la Europa, ni zawadi kwa walio dumisha imani katika msimu mgumu. Mwalimu huyo mwenye asili ya Australia, ametengeza historia pamoja na timu yake, Tottenham Hotspur, ambayo ime ishinda Manchester United kwa goli moja kwa mtungi katika fainali iliyo chezewa mjini Bilbao, Uhispania.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now