Taarifa ya Habari 26 Juni 2025

Bench - Swahili.jpg

Waziri wa fedha wa shirikisho Katy Gallagher ametetea bajeti ya ulinzi ya Australia, wakati kuna shinikizo kutoka humu ndani na kutoka ng’ambo.


Mwanamke mmoja atafikishwa mahakamani hii leo, kujibu shtuma za kudukua hifadhidata ya chuo chake katika jaribio laku okoa hela zaku egesha gari lake.

Watu 12 wameripotiwa kuuawa na wengine zaidi ya 350, wamejeruhiwa kwenye maandamano ya kuadhimisha mwaka mmoja tangu tukio la Juni 25 ambapo vijana 60 waliuawa walipokuwa wakipinga mswada wa Fedha nchini Kenya.

Mkuu wa majeshi ya Uganda Jenreali Muhoozi Kainerugaba ameamsha hasira ya wapiganaji wazalendo ambapo amechapisha katika mtandao wake wa X nia yake ya kuwalenga wapiganaji hao, ambao ni washirika wa FARDC katika maeneo kadhaa ya mashariki.

Rugby Australia inatumia akili bandia kwa umbo la app ya bure kukabiliana na unyanyaji wa mtandaoni, na unyanyasaji wa wachezaji kupitia mtandao wajamii. App hiyo hutambua moja kwa moja nakufuta maoni yenye madhara, yakuudhi na matusi kutoka akaunti ya mtandao wajamii ya mtumiaji, machapisho au kurasa kwa wakati halisi.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service