Huduma ya dharura ya jimbo [[SES]] imesema nyumba 794 katika kanda ya pwani ya kati ya kaskazini, zime zingatiwa kuwa haziwezi tumiwa tena baada ya zaidi ya tathmini 5000 za uharibifu kufanywa.
Bei za umeme za wateja wanao tumia ofa za soka, zinatarajiwa kuongezeka kwa asilimia 0.5 na asilimia 9.7 kuanzia Julai 1. Bei halisi za usalama uwekwa upya kila mwaka na msimamizi kumulika gharama ya uzalishaji na utoaji wa umeme kwa nyumba na biashara. Gharama za kuzalisha za juu na nguzo pamoja na waya, vimechangia kwa ongezeko ya bei ya 2025.
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye anaendelea kuzuiliwa, angalau hadi kufikishwa kwake tena mahakamani Mei 29, 2025. Alikamatwa mwezi Novemba mwaka jana wakati alipokuwa akisafiri nchini Kenya na kuonekana tena siku chache baadaye nchini Uganda, ambako anafunguliwa mashitaka kwa "uhaini," uhalifu unaostahili adhabu ya kifo.
Kiongozi wa muungano wa kisiasa na kijeshi wa waasi wa AFC/M23 Corneille Nangaa, ametangaza kuwa rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo Joseph Kabila amewasili katika mji wanaoudhibiti wa Goma. Corneille Nangaa amesema kwa pamoja na Kabila wanadhamiria kukomesha kile alichokiita udikteta na migawanyiko nchini Kongo.