Taarifa ya Habari 28 Februari 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Serikali ya shirikisho imetangaza mageuzi ya ushuru kwenye salio la juu ya malipo ya uzeeni. Kuanzia mwaka wa fedha wa 2025/2026, salio la zaidi ya dola milioni tatu, itatozwa ushuru wa 30% kutoka kiwango cha sasa cha ushuru wa 15%.


Chama cha Labor cha NSW kimetangaza mageuzi kwa huduma ya afya ya akili ya shirika la lifeline, nakuongeza mara mbili ufadhiliu wa huduma za mazungumzo. Tangazo hilo limejiri wakati kuna ongezeko kwa idadi yawa Australia wanao endelea kutegemea huduma za afya ya akili, hususan baada ya janga la UVIKO-19.

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi alisema Jumatatu kwamba mzozo na waasi mashariki mwa nchi hiyo unaweza kuvuruga maandalizi ya uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Desemba 20.

Mgombea wa Urais wa chama tawala nchini Nigeria, Bola Tinubu anaongoza kwa kura katika majimbo 20 kati ya 36 nchini Nigeria. Matokeo hayo ya awali ni kwa mujibu wa matokeo ya awali yaliokusanywa na shirika la habari la la Uingereza Reuters. Lakini wapinzani wamelisusia zoezi la kuhesabu kura kwa kuonesha mashaka ya vitendo vya udanganyifu.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 28 Februari 2023 | SBS Swahili