Taarifa ya Habari 30 Mei 2025

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Wakati inaweza chukua zaidi ya mwaka kwa baadhi ya madai ya bima ya mafuriko kutatuliwa, malipo ya mara moja kwa walio athirika jimboni New South Wales yata anza kutolewa leo 30 Mei 2025.


Sussan Ley amesema aina yake ya uongozi uta tofautiana na mtangulizi wake Peter Dutton, ambapo uongozi wake utalenga ksikiza badala yakutoa somo. Kiongozi huyo wa upinzani ali ambia shirika la habari la ABC, Upinzani wa mseto ambao ume badilika , pamoja na kiongozi wa Nationals David Littleproud, wana wakilisha timu imara inayo ungana.

Rais wa zamani wa DRC Joseph Kabila amekutana na viongozi wa dini Alhamis Mjini Goma, Mji Mkuu wa Kivu Kaskazini wa mashariki mwa Kongo na unaokaliwa na waasi wa M23 wanaosaidwa na Rwanda. Ziara yake imekuja wakati huu Rais huyo wa zamani akikabiliwa na kesi ya uhaini kwa madai ya kuunga mkono kundi la M23, bunge la Seneti likiwa limemuondolea kinga yake ya kutoshtakiwa ambapo sasa anaweza kufunguliwa mashtaka.

Viongozi wa Upinzani wamekataa msamaha uliotolewa na Rais William Ruto wakati wa Maombi ya Kitaifa Jumatano. Wakiongozwa na Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka ambaye alialika wenzake nyumbani kwake Tseikuru, Kaunti ya Kitui, viongozi hao walisema ombi la msamaha la Ruto lilinuiwa kufumba macho Wakenya baada ya kuhisi kwamba atashindwa kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2027. Bw Musyoka alisema ombi hilo lilikuwa kejeli kubwa kwa familia ambazo bado zinaomboleza watoto wao waliouliwa na risasi za polisi wakati wa Maandamano ya Kupinga Mswada wa Fedha 2024.

Ngugi wa Thiong'o, mwandishi maarufu na msomi kutoka Kenya, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 87. Kifo chake kimethibitishwa na mwanawe, Nducu wa Ngugi, ambaye amesema mwandishi huyo amefariki mjini Bedford, Georgia, ambako alikuwa akipokea matibabu ya figo. Ngugi alikuwa mmoja wa watu mashuhuri zaidi barani Afrika waliotumia kalamu kama silaha ya ukombozi wa kiakili na kijamii.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service