Taarifa ya Habari 4 Julai 2025

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Kamishna wa zamani wa tume yakifalme ame kosoa serikali, kwa kufeli kuchukua hatua haraka kwa mfumo wakitaifa wakufanya ukaguzi kwa ajili yakufanya kazi na watoto.


Watetezi wa haki katika wilaya ya Australian Capital Territory wamesema uamuzi wa serikali ya wilaya hiyo kuongeza umri wa uwajibikaji wa uhalifu, unastahili kuwa mfano kwa majimbo na wilaya zingine. A-C-T imekuwa mamlaka yakwanza nchini Australia kuongeza umri ambapo mtoto anaweza wajibishwa kwa uhalifu akiwa na miaka 14.

Serikali ya Tanzania imekanusha vikali tuhuma zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii na kudai kuwa zinaihusisha yenyewe na kiongozi wa upinzani, Tundu Antipas Lissu, katika mpango wa kumuwekea sumu mshtakiwa huyo. Kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa Julai 3, 2025, na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Serikali imetoa wito kwa wananchi kupuuza taarifa hizo, ikisisitiza kuwa "hazina ukweli wowote."

Watu sita waliodaiwa kuwa wachawi wameuawa kwa kupigwa, kuchomwa moto na kupigwa mawe katika kijiji cha Gasarara, kilomita chache kutoka jiji la Bujumbura, nchini Burundi. Mashuhuda wanasema shambulizi hilo lilitekelezwa na vijana wa kundi la Imbonerakure, linalohusishwa na chama tawala cha CNDD-FDD.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 4 Julai 2025 | SBS Swahili