Taarifa ya Habari 5 Juni 2025

Bench - Swahili.jpg

Marekani imetumia kura yake ya turufu dhidi ya azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, lililo kuwa likiomba kusitishwa kwa vita pamoja na misaada yakibinadam kuruhusiwa kuingia katika ukanda wa Gaza bila vizuizi.


Kuna uwezekano wakaaji wa Tasmania wana weza elekea debeni hivi karibuni, kiongozi wa jimbo hilo Jeremy Rockliff akitarajiwa kufurushwa ofisini na bunge. Serikali hiyo ya wachache ya chama cha Liberal, inakabiliwa na machafuko yakisiasa baada ya Bw Rockliff kukabiliwa kwa kura yakutokuwa na imani dhidi yake jana Jumatano 4 Juni, mjadala mrefu unatarajiwa kuendelea vikao vitakapo anza tena leo asubuhi.

Polisi jijini Dar es Salaam Tanzania wamezingira jengo la kanisa la Ufufuo na Uzima linalomilikiwa na mbunge wa jimbo la Kawe Josephat Gwajima, ambaye wiki iliyopita, alilaani matukio ya utekaji nchini humo.

Wakati huu wakikabiliwa na hali mbaya ya kiuchumi, raia wa Burundi ingawa wamechoka lakini wanajiandaa kushiriki uchaguzi mkuu wa wabunge wa Juni 5 ambao umepoteza mvuto na kukosekana kwa washindani wa kweli.

Msafara wa Hija ume anza mjini Mecca, ambako zaidi ya idadi yawa Islamu milioni 1.5 kutoka duniani kote watawasili Saudi Arabia kutekeleza wajibu wao wakidini. Tukio hilo ni moja ya nguzo tano za Uislam, wajibu wa maramoja katika maisha kwa kila Muislamu anaye weza imudu, na ana uwezo kimwili wakufanya hivyo.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service