Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 5 Machi 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri Mkuu aikosoa serikali ya NSW katika kampeni ya uchaguzi jimboni humo.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Waziri Mkuu aikosoa serikali ya NSW katika kampeni ya uchaguzi jimboni humo.


Kiongozi wa NSW Dominic Perrottet, atupilia mbali ukosoaji wa Waziri Mkuu Albanese, nakusisitiza ana amini chama chake cha NSW Liberals, kinastahili kuwa na awamu ya nne madarakani. Amesisitiza kuwa malengo yake ni kwa siku za usoni za jimbo hilo, si mashambulizi binafsi.

Serikali ya shirikisho imetoa data mpya inayo onesha maelfu yawazee nchini Australia, wamefaidi kupitia madawa ya bei nafuu pamoja naku waona ma GP, wakati mageuzi mapya yame anza kutumika. Mageuzi kwa vizingiti vya mapato kwa kadi ya afya ya shirikisho yawazee, mwezi Novemba ilipanua upatikanaji kwa wazee elfu 10,893. Vizingiti kwa watu wasio na wachumba vili inuliwa kutoka $58,000 hadi $90,000. kwa wachumba vizingiti viliongezeka kutoka $92,416 hadi $144,000.

Burundi ilitangaza Ijumaa kwamba ingepeleka wanajeshi 100 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuanzia Jumamosi, kama sehemu ya kikosi cha kikanda.

Afisa mkuu wa jeshi la Burundi aliliambia shirika la habari la AFP kwamba wanajeshi hao walikuwa tayari kuungana na wenzao wa nchi zingine za kikanda, katika operesheni hiyo. Baadhi ya mataifa saba ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yalituma wanajeshi mwishoni mwa mwaka jana mashariki mwa DRC, eneo ambalo limekuwa likipambana na kuongezeka kwa wanamgambo, wakiwemo waasi wa M23.

Majimbo sita yanayoongozwa na upinzani nchini Nigeria yameiomba mahakama ya juu kutupilia mbali matokeo ya uchaguzi wa rais uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita, wakisema chombo cha kusimamia uchaguzi kilivunja sheria na kanuni zake wakati wa kuhesabu kura, hati za mahakama zilionyesha. Mgombea wa chama tawala cha All Progressive Congress (APC) Bola Tinubu alitangazwa mshindi siku ya Jumatano, lakini wapinzani wawili kutoka vyama vikuu vya upinzani walisema matokeo hayo yalikuwa ya udanganyifu na kuapa kuyapinga mahakamani.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now