Taarifa ya Habari 6 Septemba 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Serikali ya shirikisho yashinikizwa iongeze muda wa makato ya kodi ya mawese, ambayo imeratibiwa kuisha mwisho wa mwezi huu.


Seneta huru David Pocock ameomba muda wa makato ya kodi yamawese ongezwe.
Makato hayo ya muda ya senti 22 za kodi yamawese, yameratibiwa kuisha mwisho wa mwezi huu, serikali ya shirikisho ikisema hatua hiyo haiwezi ongezewa muda kwa sababu ya shinikizo za bajeti. Wakati huo huo Benki ya Hifadhi ime ongeza viwango vya riba kwa mwezi watano mtawalio. Kiwango cha hela taslim kimefikia 0.5% kwa mwaka wa saba nakufikia 2.35%.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameahidi kuhakikisha kwamba anakabidhi madaraka kwa uongozi mpya, wa Dr. William Ruto. Katika ujumbe uliorekodiwa na kuwekwa kwenye mtandao wa You Tube, Kenyatta hata hivyo ameonekana kukosoa uamuzi wa mahakama ya juu uliotupilia mbali kesi ya kupinga ushindi wa William Ruto. Kesi hiyo iliwasilishwa na Raila Odinga wa muungano wa Azimio. Mwenyekiti wa mrengo wa Azimio ni rais Uhuru Kenyatta.

Mataifa Tajiri yamesema yatatumia karibu dola bilioni 25 ifikapo mwaka wa 2025, ili kupiga jeki juhudi za Afrika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Mkutano wa kilele wa tabia nchi ulifanyika Rotterdam, Uholanzi.



Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service