Taarifa ya Habari 7 Machi 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri Mkuu akataa kutenga gesi kwenye matumizi ya nishati, ili muswada wake uungwe mkono na chama cha Greens bungeni.


Mazingira ya joto yame endelea kushuhudiwa katika sehemu nyingi za NSW leo jumanne, moto ukiendelea kuwaka na nyuzijoto zikiendelea kupita thelathini. Bado kuna visa kadhaa vya moto ambavyo havija dhibitiwa licha ya baadhi kama moto wa Tambaroora unao waka karibu ya Bowral, ambao kiwango chake kimepunguzwa kwa tazama nakuchukua hatua.

Mafuriko yame endelea kuathiri enoe la Wilaya ya Kaskazini, barabara na madaraja yakifungwa na wakaazi wakiendelea kuwa katika vituo vya uhamisho vya dharura. Mililita mia mbili ya mvua imenyesha kati ya miji ya Alice Springs na Darwin, na vifaa vya chakula vikisafirishwa kupitia barabara mbadala na angani.

Kukosekana kwa elimu ya afya ya uzazi na vifaa tiba katika hospitali za vijijini nchini Tanzania kumetajwa kuwa ni miongoni mwa changamoto zinazo wakabili wanawake kutohudhuria kliniki hali inayo pelekea kujifungulia majumbani.

Kundi la raia wa Kongo wenye asili ya kitutsi wamekuwa wakilindwa na polisi wenye silaha wakati wakijiandikisha kupiga kura katika mji wa Nyangezi ulioko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, huku mmoja wao alilieleza kuwa kampeni za ghasia zimelenga kuwaengua katika uchaguzi ujao.



Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 7 Machi 2023 | SBS Swahili