Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE starting June 12 2026

Taarifa ya Habari 9 Februari 2024

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Uchambuzi mpya wa shirika la Regional Australia Institute umepata kuwa bei za nyumba katika maeneo ya kanda, zina fika viwango vya juu nakukaribia bei katika soko za miji.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Uchambuzi mpya wa shirika la Regional Australia Institute umepata kuwa bei za nyumba katika maeneo ya kanda, zina fika viwango vya juu nakukaribia bei katika soko za miji.


Tetemeko la ardhi lenye vipimo vya 4.3 limetikisa mji wa Melbourne na maeneo kadhaa ya Victoria. Tetemeko hilo lili fanyika mida ya saa sita hamsini usiku, na kitovu chake kilikuwa karibu ya mji wa Leongatha ambao uko katika eneo la South Gippsland.

Binti ya bibi aliye chomwa kisu hadi kufa katika kituo cha ununuzi ameomba amani, baada ya ripoti za ukatili dhidi ya jamii zawa Afrika kuibuka. Vyleen White mwenye miaka 70, alichomwa kisu hadi kufa mbele ya mjukuu wake wa kake katika eneo la Redbank Plains ambalo liko Ipswich jumamosi Feburari 4 katika kisa cha wizi wa gari. Wavulana watano wenye umri kati ya miaka 15 na 16, wamefunguliwa mashtaka kwa tukio hilo na mwingine amefunguliwa shtaka la kuuwa.

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa alitumia hotuba yake bungeni siku ya Alhamisi kuelezea mafanikio ya chama chake katika miaka 30 iliyopita, lakini akatoa maelezo machache kuhusu mipango yake ya kushughulikia changamoto kuu zinazoendelea kuikumba nchi hiyo.

Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi (ECOWAS) imesema leo kuwa mataifa ya Niger, Mali na Burkina Faso yameshindwa kuheshimu sheria kwa kujiondoa katika kundi hilo.

Kufuatia mkasa wa mlipuko wa gesi eneo la Embakasi, mjini Nairobi mwishoni mwa wiki, miji mengine sasa inachukua tahadhari ili kuepusha maafa sawia na hayo siku za usoni.

Mjini Mombasa Gavana wa jimbo hilo Abdulswamad Sharrif Nassir ameamrisha kufungwa kwa maduka na vituo vya uuzaji gesi kinyume na sheria. Washukiwa wa kiwanda cha gesi cha Embakasi, Nairobi kilichosababisha vifo vya watu saba na mamia kujeruhiwa, wakiendelea kuzuiliwa na polisi, serikali ya jimbo la Mombasa , imefunga vituo vya biashara za gesi vinavyoendeshwa kinyume na sheria.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now