Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Waziri Mkuu afanya kampeni katika wikendi ya Pasaka

Scott Morrison

Scott Morrison Source: AAP / Richard Wainwright

Waziri Mkuu anaendelea kutetea uamuzi wa chagua lake kwa mgombea wa chama cha Liberal, kwa eneo bunge la Warringah ambalo liko mjini Sydney.


Published

Updated

By Claire Slattery, Pablo Vinales

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Waziri Mkuu anaendelea kutetea uamuzi wa chagua lake kwa mgombea wa chama cha Liberal, kwa eneo bunge la Warringah ambalo liko mjini Sydney.


Taarifa zimeibuka kuwa Katherine Deves alitoa madai mtandaoni yakibaguzi dhidi ya watu wenye jinsia tofauti, kauli ambayo ameombea msamaha. Wakati huo huo upinzani ume apa kuanzisha tume ya uchunguzi wa ufisadi wa shirikisho kufikia mwisho wa mwaka huu ukishinda uchaguzi mkuu.

Tukisalia katika maswala ya kampeni, mbunge wa chama cha Labor Chris Bowen alikuwa anatarajiwa kujiunga na kampeni ya Bw Albanese jimboni Queensland ila, amelazimishwa kuingia katika karantini baada ya vipimo vyake vya UVIKO-19 kurejesha matokeo chanya. Bw Bowen ni mbunge wa tatu aliye ambukizwa wiki hii, baada ya msemaji wa maswala ya nyumbani katika chama cha Labor Kristina Keneally na Waziri wa maswala ya nyumbani Karen Andrews.

Kampeni hizo zilisitishwa kwa sababu ya Pasaka ya Jumapili.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now