Waziri Mkuu afanya kampeni katika wikendi ya Pasaka

Scott Morrison

Scott Morrison Source: AAP / Richard Wainwright

Waziri Mkuu anaendelea kutetea uamuzi wa chagua lake kwa mgombea wa chama cha Liberal, kwa eneo bunge la Warringah ambalo liko mjini Sydney.


Taarifa zimeibuka kuwa Katherine Deves alitoa madai mtandaoni yakibaguzi dhidi ya watu wenye jinsia tofauti, kauli ambayo ameombea msamaha. Wakati huo huo upinzani ume apa kuanzisha tume ya uchunguzi wa ufisadi wa shirikisho kufikia mwisho wa mwaka huu ukishinda uchaguzi mkuu.

Tukisalia katika maswala ya kampeni, mbunge wa chama cha Labor Chris Bowen alikuwa anatarajiwa kujiunga na kampeni ya Bw Albanese jimboni Queensland ila, amelazimishwa kuingia katika karantini baada ya vipimo vyake vya UVIKO-19 kurejesha matokeo chanya. Bw Bowen ni mbunge wa tatu aliye ambukizwa wiki hii, baada ya msemaji wa maswala ya nyumbani katika chama cha Labor Kristina Keneally na Waziri wa maswala ya nyumbani Karen Andrews.

Kampeni hizo zilisitishwa kwa sababu ya Pasaka ya Jumapili.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Waziri Mkuu afanya kampeni katika wikendi ya Pasaka | SBS Swahili