Farewell Mr Football

Jamii ya kandanda nchini Australia imepokea kwa huzuni ujumbe kuwa, wame mupoteza mtangazaji maarufu wa SBS na kandanda Les Murray.

Les Murray akiwa katika uwanja wa kandanda mjini Sydney, Australia

Les Murray akiwa katika uwanja wa kandanda mjini Sydney, Australia Source: SBS

Les alikuwa mmoja wa watu walio kuza kandanda nchini Australia, akishirikiana na rafiki yake wa karibu ambaye pia alikuwa mchezaji wa zamani wa Australia Johnny Warren.

Les Murray na Johnny Warren wazindua kitabu chao "Mr & Mrs Soccer"
Les Murray na Johnny Warren wazindua kitabu chao "Mr & Mrs Soccer" Source: Getty Images AsiaPac
Hatakama rafiki yake haku fanikiwa kushuhudia Australia ikikabiliana na vigogo wa soka katika kombe la dunia baada ya miaka mingi ndani ya jangwa la soka, Les Murray aliongoza matangazo ya soka kwa ufanisi ndani ya nyumba zawa Australia kila siku.
Mtangazaji wa soka Australia, Les Murray
Mtangazaji wa soka mstaafu wa SBS Australia, Les Murray Source: The World Game

Les aliongoza matangazo ya soka kwa mara ya mwisho katika michuano ya kombe la dunia ya FIFA nchini Brazil mwaka wa 2014. Aliwaaga watazamaji kwa mara ya mwisho akizungukwa na marafiki na washiriki, pamoja naku acha urithi utakao wa faidi waandishi wa habari kwa miaka mingi ijayo.

Mtangazaji wa soka wa SBS Australia, Les Murray akiaga watazamaji kwa mara ya mwisho
Mtangazaji wa soka wa SBS Australia, Les Murray akiaga watazamaji kwa mara ya mwisho Source: The World Game

Hata kama jamii ya kandanda ya Australia imempoteza mwanao mpendwa, hakuna shaka urithi wake uta ishi nakudumu milele.


Share

1 min read

Published

Updated

By SBS Swahili

Presented by SBS Swahili

Source: SBS Swahili




Share this with family and friends