Forodha kwa ujumla ndio sehemu ya kwanza ya mawasiliano kwa watu wanaoingia Australia. Maafisa wa Kikosi cha Mpakani cha Australia wako tayari kwenye lango, wakilenga kuweka bidhaa zilizopigwa marufuku nje ya nchi.
Hatua kali za usalama wa kibiolojia za Australia, zimewekwa kwa ajili yakulinda mazingira yetu ya kipekee, uchumi na jamii.
Kabla ya kufunga mzigo wako, haya ndiyo unayohitaji jua kuhusu kile kinachoweza na kisichoweza vuka mpaka, na kile kilicho hatarini kama sheria za usalama wa kibiolojia zitapuuzwa.
Orodha kamili ya bidhaa zilizopigwa marufuku inapatikana kwenye tovuti ya Kikosi cha Mpakani cha Australia.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.





