Mjadala unaendelea kuhusu mustakabali wa mfumo wa kodi wa Australia, baada yakutolewa kwa bajejeti ya Shirikisho wiki iliyopita.
Upinzani wa Mseto umetangaza sera zake zisizo za kawaida kuhusu kodi na nyumba, wakati Mweka Hazina anafanya kazi kuuza mabadiliko matatu yanayoathiri ugawaji hasi, faida za mtaji na mifuko ya uaminifu.
Kura mbili mpya za maoni zinapendekeza kwamba bajeti yake ya shirikisho haijapokewa vizuri na wapiga kura - lakini Jim Chalmers ametangaza kwamba manufaa ya muda mrefu yanayotokana na mabadiliko ya kodi ya nyumba yenye utata yanastahili maumivu ya muda mfupi ya kisiasa.





