Hali hii inafuatia maoni ya Kamishna wa Polisi wa Shirikisho mwishoni mwa mwaka jana, akibainisha mwenendo wa kuongezeka kwa vurugu dhidi ya maafisa wa umma.
Kufuatia tisho la bomu lililotolewa kwa lugha ya Mandarin dhidi yake na maafisa wengine wakuu, Waziri Mkuu Anthony Albanese alihamishwa kwa masaa kadhaa kutoka makazi yake ya Canberra siku ya Jumanne.
Madai ya uongo yalitolewa kwamba vilipuzi vilikuwa vimetegwa ili kulipua makazi ya Waziri Mkuu kuwa magofu, siku chache kabla ya onyesho lililopangwa kufanywa na kundi la Shen Yun Performing Arts.
Kampuni hiyo ya densi yenye makao yake makuu mjini New York imekuwa ikikosoa chama cha kikomunisti cha China, na imepigwa marufuku nchini China. Kampuni hiyo inakabiliwa na shinikizo na madai yanayoendelea ya kufuta maonyesho yake ya kimataifa.
Bonyeza hapo juu kwa makala kamili.





