Lionel Messi amekuwa mfungaji bora wa muda wote wa Kombe la Dunia, akifunga mara mbili nakusaidia Argentina kuishinda Austria 2-0 mjini Dallas, na kujihakikishia nafasi ya kwanza katika Kundi J, pamoja na nafasi katika hatua ya mchujo.
Sikiliza makala yetu yaliyo rekodiwa hapa
Katika Kundi I, Timu ya Iraq inayo ongozwa na Mwalimu Graham Arnold, ilipata kichapo cha magoli 3 dhidi ya Ufaransa mjini Philadelphia, Kylian Mbappé aki adhimisha mechi yake ya kimataifa ya 100 kwa kufunga bao mbili. Mechi hiyo iliahirishwa kwa zaidi ya masaa mawili kwa sababu ya hali mbaya ya hewa, mara ya kwanza kwa mashindano hayo kukatizwa na hali ya hewa.
Wakati Australia ikijiandaa kwa pambano lake la mwisho la kundi lao dhidi ya Paraguayi katika Kombe la Dunia, Waziri Mkuu Anthony Albanese ame hamasisha taifa kuwaunga mkono Socceroos, akiisifu timu hiyo kama kielelezo cha utofauti na moyo wa Australia.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






