Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari: 13 wauawa katika milipuko Burundi

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Ushuru wa petroli unatarajiwa kupunguzwa zaidi, wakati viongozi wa majimbo na wilaya wakikubaliana kuhusu mpango wa kurejesha mapato ya ziada ya ushuru wa bidhaa na huduma kutokana na kupanda kwa bei za mafuta.


Watetezi wa wahamiaji na wakimbizi wanasema jamii zilizo katika mazingira magumu, zinapuuzwa katika mwitikio wa serikali kwa athari za kiuchumi za vita katika Mashariki ya Kati.

Nchini Burundi, siku 2 baada ya kutokea milipuko katika kituo kikuu cha kuhifadhi silaha cha jeshi huko Bujumbura, Jeshi lilitangaza idadi rasmi ya awali ya raia 13 waliouawa na wengine 54 kujeruhiwa na wanajeshi watatu waliouawa. Serikali bado haijatoa taarifa.

Nchini Rwanda, kundi la watu 214 wanaohusishwa na makundi ya waasi, ikiwa ni pamoja na FDLR kulingana na mamlaka, wamerejeshwa katika maisha ya kiraia baada ya miezi kadhaa katika kituo walikkokuwa wamekusantwa kwa ajili ya kupewa maadili ya namna ya kuishi upya na raia. Miongoni mwao ni wapiganaji pamoja na raia wanaohusishwa na makundi haya.

Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now