Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 24 Machi 2026

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Australia inatafuta kupata uhakikisho wa usambazaji wa nishati kutoka kwa washirika wa biashara wakati kukiwa ongezeko la hofu kuwa nchi zitahifadhi mauzo ya nje ya mafuta kwa ajili ya masoko yao ya ndani.


Serikali ya New South Wales imesema wapangaji milioni mbili wanatarajiwa kunufaika na mfumo wa kidijitali wa kuhamisha dhamana yao kati ya nyumba za kupanga. Mfumo mpya wa teknolojia umejaribiwa ili kurahisisha uhamishaji wa kidijitali [[kupitia jukwaa lililopo la Rental Bonds Online]], na kupunguza ucheleweshaji wa kusubiri kurejeshewa dhamana, jambo ambalo linaweza kuwaacha watu bila kuwa na $4,000.

Maafisa bado wanahubiri tahadhari kwa wakazi wa Katherine katika Eneo la Kaskazini, licha ya ishara kwamba huenda wameepuka wimbi la pili la mafuriko yaliyosababishwa na Kimbunga chaki Tropiki cha Narelle. Hapakuwa mvua kubwa usiku kucha, kwa sababu kimbunga hicho cha kitropiki kinaelekea Magharibi mwa Australia.

Chama cha wanasheria nchini Uganda, ULS, kimeishtaki serikali ya Uganda kwa kile chama hicho kimesema polisi kuendelea kuzingira makazi ya mwanasiasa wa upinzani, Robert Kyagulani, maarufu kama Bob Wine. Katika kesi waliyofungua Machi 16, wanasheria wa chama hicho wanavituhumu vikosi vya usalama kuendelea kusigina katiba na sheria za nchi kwa kuzingira makazi ya Bob Wine, tangu kumalizika kwa uchaguzi wa mwezi Januari mwaka huu. Tangu kufanikiwa kuwatoroka polisi baada ya uchaguzi wa Januari 15, polisi wamekuwa wakikataza ndugu, marafiki, viongozi wa chama na hata mawakili kuingia ndani ya nyumba yake, hata kwa kupeleka chakula.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now