Taarifa ya Habari 31 Julai 2025

Bench - Swahili.jpg

Wanafunzi milioni tatu nchini Australia wata punguziwa deni zao za elimu, hii ni baada ya muswada wa Labor ulio tazamiwa sana kupitishwa bungeni hii leo.


Serikali ya Albanese iliwasilisha muswada wa deni ya HECS, waku kata asilimia 20 kutoka deni zilizopo za chuo na TAFE, kama hatua yake ya kwanza ya biashara wiki jana. Sheria hizo zina lenga kupunguza madeni ya wanafunzi, pamoja nakufanya mageuzi kwa mfumo wa malipo.



Muda wausafiri kwa treni bila malipo mjini Sydney, ume ongezwa kwa siku moja hadi asubui ya Jumamosi.Kuanzia leo hadi wikiendi, abiria watatumia huduma za treni na metro mjini Sydney bure, katika hatua yaku kiri miezi ya usumbufu ulio sababishwa na migomo.



Israel iko chini ya shinikizo kuregeza janga lakibinadam linalo endelea Gaza, Canada ikiwa nchi mpya ambayo imechukuwa hatua yakutambua utaifa wa Palestina, na mjumbe wa Marekani akiwa njiani kuelekea Mashariki ya Kati. Mwakilishi huyo wa serikali ya Trump, Steve Witkoff, anatarajiwa kuwasili nchini Israel leo, kwa mazungumzo kuhusu hali inayo endelea Gaza.



Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Uganda Robert Kyagulanyi Ssntenamu, almaarufu kama Bobi Wine amesema mazingira ya kisiasa nchini humo yamekuwa mabaya zaidi kuelekea uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika mapema mwaka 2026. Kwenye mahojiano na shirika la habari la AP kwenye makao makuu ya chama chake cha National Unity Platform, mjini Kampala, Bobi Wine amesema kumekuwa na vitisho dhidi ya maisha yake na wanaharakati wengine wanaohamasisha upinzani dhidi ya rais aliyekaa muda mrefu nchini humo Yoweri Museveni.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service