Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 4 Agosti 2025

Bench - Swahili.jpg

Serikali ya shirikisho imetangaza msaada kwa Gaza uta ongezwa kwa $20 milioni hii leo Jumatatu 4 Agosti, masaa machache baada yamakumi yama elfu kutembea katika Daraja maarufu la bandari ya Sydney, jana Agosti 3, katika maandamano dhidi ya vita vinavyo endelea Gaza.


Tazama makala yetu yaliyo rekodiwa hapa

Miaka mitano ya uhai wa bunge la 12 la Tanzania, ulitamatika Jumapili ya wikendi iliopita kufuatia tangazo la rais Samia Suluhu Hassan, kulivunja bunge hilo kwa mujibu wa katiba. Kuvunjwa kwa bunge hilo kunafungua ukurasa mwingine kwa vyama vya siasa kuanza kuteua wagombea wa nafasi za ubunge kuelekea uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka huu.

Timu ya taifa ya Kenya Harambee Stars imepata ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwenye mechi yao ya ufunguzi ya Kundi A iliyochezwa kwenye uwanja wa Moi Kasarani, jijini Nairobi. Rais William Ruto amewaahidi wachezaji wa Harambee Stars shilingi milioni 600 iwapo timu hiyo itachukua ubingwa wa CHAN mwaka huu, pamoja na shilingi milioni moja kwa kila mchezaji kwa kila ushindi wa mechi katika michuano hiyo.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now