Taarifa ya Habari 4 Agosti 2025

Bench - Swahili.jpg

Serikali ya shirikisho imetangaza msaada kwa Gaza uta ongezwa kwa $20 milioni hii leo Jumatatu 4 Agosti, masaa machache baada yamakumi yama elfu kutembea katika Daraja maarufu la bandari ya Sydney, jana Agosti 3, katika maandamano dhidi ya vita vinavyo endelea Gaza.


Miaka mitano ya uhai wa bunge la 12 la Tanzania, ulitamatika Jumapili ya wikendi iliopita kufuatia tangazo la rais Samia Suluhu Hassan, kulivunja bunge hilo kwa mujibu wa katiba. Kuvunjwa kwa bunge hilo kunafungua ukurasa mwingine kwa vyama vya siasa kuanza kuteua wagombea wa nafasi za ubunge kuelekea uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka huu.

Timu ya taifa ya Kenya Harambee Stars imepata ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwenye mechi yao ya ufunguzi ya Kundi A iliyochezwa kwenye uwanja wa Moi Kasarani, jijini Nairobi. Rais William Ruto amewaahidi wachezaji wa Harambee Stars shilingi milioni 600 iwapo timu hiyo itachukua ubingwa wa CHAN mwaka huu, pamoja na shilingi milioni moja kwa kila mchezaji kwa kila ushindi wa mechi katika michuano hiyo.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service