Waziri Mkuu Anthony Albanese anasema serikali lazima zishughulikie mfadhaiko katika uchumi unaoongezeka, baada ya kura mpya ya maoni kuonyesha ongezeko la uungwaji mkono kwa chama cha One Nation.
Sikiliza makala yetu yaliyo rekodiwa hapa
Kura hiyo ya maoni inajiri huku kukiwa na mjadala kuhusu mageuzi ya kodi yaliyopendekezwa na Labour, ambayo yanakabiliwa na upinzani kutoka kwa Upinzani wa Mseto Muungano na bado hayajapata uungwaji mkono kutoka kwa chama cha Green.
Aliyekuwa Naibu Rais nchini Kenya Rigathi Gachagua amepata pigo kubwa mahakamani, baada ya jopo la majaji watatu kutupilia mbali kesi ya kupinga kutimuliwa kwake serikalini. Katika uamuzi wa majaji Freda Mugambi, Anthony Mrima na Eric Ogolla, walisema kwamba sheria zilifuatwa katika mchakato mzima wa kumtimua Bw Gachagua uongozini.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






