Waziri Mkuu Anthony Albanese haja tupilia mbali uwezekano wa kuongeza muda wa kupunguzwa kwa ushuru wa mafuta kutokana na kufufuliwa upya kwa mapigano Mashariki ya Kati.
Shirika la kimataifa la haki za binadamu la Human Rights Watch inawashutumu waasi wa M23 na jeshi la Rwanda kwa kulazimisha watu wengi kuajiriwa jeshini, kunyongwa, na vifo katika kambi mbili za kijeshi huko Kivu Kaskazini. Katika ripoti yake, shirika hilo lisilo la kiserikali pia linaikosoa serikali ya Kongo, likiishutumu kwa kuunga mkono makundi yenye silaha yanayohusika na unyanyasaji mkubwa. Shirika hilo linavitaja vitendo hivi kama uhalifu wa kivita.
Alex de Minaur ameshinda mechi yake ya kwanza baada ya kurejea kwake katika uwanja wa nyasi, baada ya kuonyesha kiwango cha kutoridhisha katika uwanja wa udongo kwenye mchezo wa wazi wa Ufaransa. Na Mexico na Afrika Kusini zasubiri kipenga cha mwamuzi, kuanza Kombe la Dunia la FIFA la 2026.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.





