Bei ya petroli imeshuka hadi viwango ambavyo havijaonekana tangu mwanzo wa 2022. Taasisi ya Petroli ya Australia inasema wastani wa kitaifa wa lita moja ya mafuta yasiyo na risasi ulishuka zaidi ya senti 6 wiki iliyopita - hadi chini kidogo ya dola 1.60.
Sikiliza makala yetu yaliyo rekodiwa hapa
Mamilioni ya Waustralia wataamka kesho [[Julai 1]] kwa mishahara ya juu na kodi ya chini ya mapato, huku mwaka mpya wa fedha ukileta mabadiliko mbalimbali kwa wafanyakazi na familia. Karibu wafanyakazi milioni 2.8 wanaolipwa mishahara ya chini na ya tuzo watapata nyongeza ya mishahara kutoka kipindi chao cha kwanza cha malipo kamili kuanzia tarehe au baada ya tarehe ya kwanza ya Julai.
Nchini Afrika Kusini, ghasia dhidi ya raia wa kigeni zinazidi kushika kasi. Wachambuzi wanasema serikali ilishindwa mapema kukabiliana na chuki dhidi ya wageni na kutatua matatizo ya kijamii yanayochochea hali hiyo. Serikali imesema imejipanga kukabiliana na mlipuko wowote wa ghasia. "Hatutaruhusu jaribio lolote la kuivuruga nchi yetu, kutoka kwa yeyote, iwe wanaandamana au la," Rais Cyril Ramaphosa alisema Alhamisi.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.






