Waziri wa Mambo ya Nje Penny Wong atajiunga na wenzake kutoka nchi 35, ikiwa ni pamoja na Italia, Ufaransa, Ujerumani na Japani, katika mkutano wa mtandaoni. Marekani haijaalikwa.
Waziri Mkuu anatarajiwa kutangaza usaidizi zaidi wa kifedha kwa biashara zilizoathiriwa na mzozo wa mafuta duniani.
Anatarajiwa kutangaza unafuu wa ulipaji wa mikopo wa dola bilioni 1 chini ya Mpango wa Serikali wa Ustahimilivu wa Kiuchumi, ambao serikali inasema utamaanisha kuwa malori, makampuni ya mizigo, na wazalishaji wa mafuta na mbolea watasaidiwa vyema ili kuendelea na kazi muhimu. Katika hotuba ya kitaifa jana usiku, Anthony Albanese alihimiza utulivu, lakini alionya kwamba kunaweza kuwa na nyakati ngumu mbele.
Wakazi wa jamii za kaskazini mwa Queensland zilizokumbwa na kimbunga Narelle wiki iliyopita wanaweza kukabiliwa na kimbunga kingine wiki ijayo. Wataalamu wa hali ya hewa wanafuatilia mfumo wa hali ya hewa ya chini ya kitropiki, unaounda kando ya Visiwa vya Solomon ambao unaweza kuwa kimbunga ifikapo Jumapili 5 Aprili.
Tisho hilo halikaribishwi kwa mamia ya watu ambao bado wanafanya usafi kutokana na uharibifu wa Kimbunga Narelle - huku kimbunga cha kiwango cha nne kikigonga sehemu ambazo tayari zimefurika za Wilaya ya Kaskazini na Queensland wiki iliyopita.
Milipuko kadhaa imesikika kwenye mji mkuu wa Burundi, Bujumbura, baada ya moto kuzuka kwenye ghala za silaha la kambi moja ya kijeshi mjini humo. Milipuko hiyo ilizusha taharuki kwenye maeneo mbalimbali ya mji huo wenye wakaazi zaidi ya milioni moja, huku kombora moja likiangukia karibu na kituo cha redio cha taifa.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.





