Jeshi la Polisi la Shirikisho la Australia limemkamata mwanamke mmoja, kama sehemu ya uchunguzi unaoendelea chini ya Operesheni Kurrajong.
Mwanamke huyo anashtakiwa na Kikosi Kazi cha Pamoja cha Kupambana na Ugaidi cha AFP lakini asili ya mashtaka hayo bado hayajulikani. Ina ripotiwa kuwa mwanamke huyo amerejea Australia hivi karibuni.
Wabunge wa chama cha Labor wanatetea mageuzi ya kodi yaliyopendekezwa na serikali, ambayo yanatarajiwa kupitishwa bungeni kwa kuungwa mkono na chama cha Greens. Msaidizi wa mweka hazina Daniel Mulino anasema serikali inasonga mbele kutoa ufafanuzi haraka iwezekanavyo. Wakati huo huo Kiongozi wa Upinzani Angus Taylor anasema, ingawa mageuzi ya kodi yanahitaji kufanyika - mapendekezo ya Mweka Hazina si sahihi.
Kituo cha udhibiti na kuzuia magonjwa Afrika CDC, kimesema kuwa kimeongeza juhudi za kinga na kuharakisha maendeleo ya chanjo kufuatia mlipuko wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Jean Kaseya, alisema siku ya Jumanne kuwa hatua hizo mpya zinachukuliwa ili kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa huo na kuzuia athari zake kuongezeka katika ukanda huo.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.






