Upinzani wa Mseto unakosoa muswada wa mageuzi ya kodi wa serikali ya Labour, kwa kumpa mweka hazina mamlaka ya kuamua ni mali gani zinaweza wekewa punguzo la kodi ya faida ya mtaji.
Chini ya rasimu ya sheria hiyo, Mweka hazina anaweza kuamua ni mali gani zinaweza kuruhusiwa kuhifadhi punguzo la Kodi ya Faida ya Mtaji, ni malipo gani ya usaidizi wa mapato ambayo yatapewa msamaha kutoka kwa CGT ya chini kabisa na ni mali gani zilizoainishwa kama "majengo mapya".
Vijana katika kaunti ya Laikipia wapinga hatua ya serikali ya kujenga kituo cha kupokea wagonjwa wa Ebola raia wa Marekani. Mamia ya vijana katika mji wa Nanyuki nchini Kenya leo wamejitokeza katika maandamano ya kupinga hatua ya serikali ya kuruhusu kujengwa kituo cha kupokea wagonjwa wa Ebola raia wa Marekani, katika kambi ya jeshi ya Laikipia. Maandamano hayo yanashuhudiwa siku mbili baada ya mahakama kuu ya Kenya kutoa agizo la kusitishwa ujenzi wa kituo hicho pamoja na kuzuiwa kuingia raia wa kigeni walioambukizwa virusi hivyo, hadi itakaposikilizwa kesi iliyowasilishwa na chama cha wanasheria nchini Kenya na taasisi inayosimamia katiba.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.






