Watch FIFA World Cup 2026™ LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari: Upinzani waikosoa Serikali ya Madola kwa kuto fanya yakutosha kuimarisha usalama wa taifa

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS / SBS Swahili

Mbunge wa Upinzani Jonathon Duniam amesema Serikali ya shirikisho lazima iende mbali zaidi ili kuimarisha usalama wa taifa, kufuatia kutolewa kwa ripoti ya muda iliyotolewa na Tume ya Kifalme inayochunguza maswala ya chuki dhidi ya wayahudi na Uwiano wa Kijamii.


Licha ya ukosoaji huo Waziri Mkuu amepuuza ufichuzi katika ripoti ya tume ya muda ya kifalme kwamba, matumizi ya fedha katika kupambana na ugaidi 'yalipungua kwa kiasi kikubwa' kabla ya shambulio la kigaidi la Bondi. Ripoti hiyo imetoa mapendekezo 14 ikiwa ni pamoja na usalama zaidi katika matukio ya Kiyahudi, mapitio ya mifumo ya ujasusi ya Australia na sheria thabiti za kitaifa za bunduki. Licha ya kupendekeza mapitio ya mifumo iliyopo, jaji wa zamani wa Mahakama Kuu Virginia Bell, na mkuu wa tume amesema hakuna suala linalohitaji hatua za haraka lililotambuliwa.

Shirika la Anglicare Australia linasema uwezo wa kukodisha nyumba umepungua kwa kiwango cha chini kabisa. Picha yake ya hivi karibuni ya Uwezo wa Kukodisha Nyumba iliyofanyiwa utafiti ilifikia takriban orodha elfu 49 kote nchini, ikibaini kuwa kukodisha nyumba moja tu nchini kote kulikuwa nafuu kwa mtu anayetumia JobSeeker, na hakuna kwa mtu anayetumia Posho la vijana. Mtendaji mkuu wa shirika la Anglicare Australia Kasy Chambers, anasema swala la nyumba lazima lichukuliwe kama haki ya msingi.

Mwanamume mwenye uraia wa Uganda na Marekani, Christopher Okello Onyum, ambaye aliwaua kwa kuwachoma visu watoto wanne katika kituo cha kulelea watoto wachanga mapema mwezi huu, amehukumiwa adhabu ya kifo na mahakama jijini Kampala. Mauaji hayo ya kutisha yameibua wito wa kuimarishwa kwa usalama katika shule na vituo vya kulelea watoto ili kuzuia matukio kama hayo yasijirudie.


Share

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Watch now