Kila mwaka, maelfu ya wahitimu wa shule nchini Australia husafiri nje ya nchi kwa mapumziko, kwa tukio linalojulikana kama "schoolies". Ni wakati ambapo vijana huanza safari zao za kimaisha - na wazazi hufanya dua. Kwa Michelle Jones, ambaye binti yake Bianca hakurudi kutoka likizo yake Laos, ni kumbukumbu yenye machungu na furaha.
Ni dhahiri sana, hasa kwenye lango la kuondoka pale ambapo tulisema kwa heri kwa wasichana wetu. ni dhahiri sana, inasikitisha sanaMichelle Jones
Bianca Jones na rafiki yake Holly Bowles walifariki baada ya kunywa vinywaji vilivyotiwa methanoli katika hosteli ya wasafiri mjini Vang Vieng, mwezi Novemba uliopita. Walikuwa na umri wa miaka 19
Sasa, wazazi wao wanataka vijana wengine wajue hatari zinazokuja na kusafiri - na kunywa pombe - nje ya nchi. Mama wa Holly, Sam Bowles, anasema wanataka kuungana na wazazi wengine.
Inatugusa sana. Tunachojaribu kufanya ni kusambaza ujumbe ili kuwalinda wasafiri wengineSam Bowles
Familia ziko katikati ya kampeni mpya ya usalama inayowalenga wanafunzi wanaohitimu shule, iliyoanzishwa na serikali ya shirikisho katika ukumbi wa kuondoka wa kimataifa wa uwanja wa ndege wa Melbourne. [[Jumanne]]
Bianca na Holly walikuwa na furaha kuhusu kusafiri nje ya nchi pamoja. Wakati Bianca aliwasilisha wazo hili kwa Mark na mimi, tulikuwa na tahadhari kidogo, lakini pia tulijua kwamba kusafiri nje ya nchi na Holly ilikuwa jambo walilotaka kufanya na tulikuwa na uhakika kuhusu wao kusafiri pamoja. Walikuwa werevu na walijua jinsi ya kujitunza.Sam Bowles
Kampeni hii inawapa vijana na wazazi ushauri wa vitendo kuhusu kunywa kwa kiasi, kutunza marafiki, na hatari zinazoweza kutokana na vinywaji visivyolipishwa, vya bei nafuu au vinavyotia shaka.
Kuwa na tahadhari kuhusu matumizi ya pombe na vinywaji vyenye kama vile cocktails, buckets na shotsSam
Kuna mwongozo wa jinsi ya kupata msaada mambo yakienda vibaya.
Inaungwa mkono na tovuti ya SmartTraveller na kikundi kisicho cha faida cha Drinkwise. Ujumbe utajumlisha matukio ya matangazo kwenye maeneo ya kuondokea katika viwanja vya ndege, na matangazo yanayolengwa kwa simu za rununu, kama anavyoeleza Mkurugenzi Mkuu wa DrinkWise, Simon Strahan.
Watakuwa wakiona hizo jumbe katika na kandokando ya viwanja vya ndege. Watakuwa wakiona hizo jumbe kwenye mitandao ya kijamii wanapotafuta baa. Itaonekana kama sehemu ya shughuli za utafutaji. Huko Australia, tutakuwa na jumbe hizo kwenye maduka ya pombe pia. Tunayo uhamasishaji, ambao utakuwa viwanjani, sehemu ya hiyo itakuwa ni kuhusika moja kwa moja na wahitimu wa shule, kuwapa bidhaa, vikumbusha vya sasa, na kweli kuanza kuzungumza naoSam Trahan
Kwa kufikia mwishoni mwa mwaka, kampeni inaongezeka kabla ya sherehe za wanaosherehekea kumaliza shule. Maelfu ya wanafunzi wanatarajiwa kusafiri ndani na nje, kwenda kwenye maeneo maarufu ya karamu kama Bali, Fiji, Gold Coast, na Asia.
Waziri wa Elimu Jason Clare anasema kampeni hii ni kuhusu kuwafikia vijana popote walipo.
Tunataka muwe na furaha na tunataka muwe salama. Tunataka mrudi nyumbani salama, na hilo ndilo msingi wa kampeni hii - taarifa mtandaoni, kwenye ndege, katika uwanja wa ndege, ujumbe wa maandishi, mitandao ya kijamii, lakini pia kufikisha taarifa kwa shule.Jason Clare
Licha ya uchunguzi mrefu na harakati za polisi huko Laos pamoja na shinikizo kutoka kwa mamlaka za Australia, bado hakuna mashtaka yaliyowekwa kuhusu vifo vya Bianca na Holly.
Michelle Jones na Sam Bowles wanakumbuka furaha ya binti zao wakati walipoanza safari yao ya kusisimua, lakini wanawasihi wazazi kuongea na watoto wao kuhusu kubaki makini.
"Wazazi wanapaswa kuwa na mazungumzo na kuwakalisha chini watoto wao, kabla ya kwenda zao.Michelle Jones na sam Bowles






