Rais wa Kenya, William Ruto, amesema serikali yake inafanya jambo sahihi kwa kuruhusu Marekani kujenga kituo cha karantini ya Ebola nchini humo.
Sikiliza makala yetu yaliyo rekodiwa hapa
Waziri wa Afya, Aden Duale naye amerudia kauli hiyo bungeni jana, ambako ali sisitiza kuwa "serikali haita shauriana na raia kuhusu uamuzi wa ujenzi wa kituo cha karantini cha Ebola nchini humo".
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameanza ziara ya siku tatu nchini Urusi ambako amekutana na Rais Vladimir Putin. Ziara hiyo inafanyika wakati Tanzania ikikabiliwa na ukosoaji kutoka mataifa ya Magharibi na mashirika ya haki za binadamu kuhusu madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu baada ya uchaguzi wa mwaka jana.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa zaidi.





