Mashabiki ulimwenguni kote wana omboleza kifo cha kigogo wa muziki wa kiafrika Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba maarufu kama Papa Wemba.
Msanii huyo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, alikuwa maarufu katika micharazo ya muziki wa Soukous na Rumba. Alifariki Jumapili asubuhi baada ya kuanguka kwenye jukwaa mjini Abidjan, Ivory Coast. Alikuwa na umri wa miaka 66.
SBS Swahili ilizungumza na Bw Blaise Itabelo ambaye ni mmoja wa maelfu wa mashabiki wa muziki wa Papa Wemba wanao ishi Australia.
Share





