Vikundi vya wafanyabiashara vinaihimiza serikali ya shirikisho kushirikiana nao, katika mashauriano kabla ya mabadiliko yoyote makubwa kutangazwa kuhusu sera ya uhamiaji.
Waziri wa Uchukuzi wa Shirikisho Catherine King ameahidi kushughulikia "masuala yoyote ya kimfumo" ambayo yanatokana na uchunguzi kuhusu jinsi ndege mbili zilivyokaribia kugongana katika Uwanja wa Ndege wa Sydney Jumapili 9 Agosti.
Mahakama mjini Malindi imetoa uamuzi kwamba uchaguzi mkuu ujao wa Kenya unapaswa kufanyika Jumanne, Agosti 11, 2026, na si mwaka wa 2027.
Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.
Share






