Serikali ya shirikisho imekuwa chini ya shinikizo la kufafanua malengo yake kuhusu mipaka ya visa, Waziri wa Mambo ya Ndani Tony Burke akiahirisha hotuba ya Klabu ya Kitaifa ya Waandishi wa Habari mwezi Agosti ambako alitarajiwa kutangaza kupunguzwa kwa uhamiaji.
Upinzani wa Victoria umevunja ahadi yake ya kuunga mkono sheria ya serikali ya kufanyia kazi kutoka nyumbani, baada yakumuunga mkono mbunge wa chama cha Shooters Fishers and Farmers kupeleka muswada huo kwa uchunguzi wa bunge. Mwanasheria Mkuu Kivuli James Newbury hapo awali alisema upinzani unaunga mkono marekebisho ya serikali, na hautapinga muswada huo ambao ungewahakikishia wafanyakazi haki ya kufanya kazi kutoka nyumbani siku mbili kwa wiki.
Kiongozi wa upinzani wa chama cha EciDe na kiongozi wa muungano wa kisiasa wa Lamuka nchini DRC, Martin Fayulu, amehoji kitendo cha Serikali kujadiliana na waasi wa AFC-M23 huko Doha lakini ikawaondoa katika orodha ya wadau wa kitaifa watakaoshiriki mazungumzo ya kitaifa yaliyotangazwa na Rais Felix Tshisekedi. Akihojiwa na redio ya umoja wa Mataofa 'RadioOkapi', Fayulu amesema njia pekee ya mazungumzo hayo kufanikiwa ni kwa wadau wote kushirikishwa.
Bofya hapo juu kwa taarifa zaidi.






