Burundi imeanzisha mfumo mpya wa kutoza kodi baada ya kuasisi Mamlaka ya kukusanya mapato nchini humo maarufu OBR kwa ufupi. Hata hivo , sehemu kubwa ya wafanyabiashara wanalalamikia mfumo huo kwamba umekuwa na viwango vikubwa vya kodi kiasi ya kutatiza shughuli zao za kibiashara. Serikali ya Burundi kupitia Ofisi ya mapato wanasema hoja za wafanyabiashara hazina msingi. Tatizo na vile wafanyabishara walizowea miaka mingi kukwepa kodi au kupitisha bidhaa zao mlango wa nyuma. Hali hiyo ya mvutano imesababisha biashara nyingi kusalia katika ghala za bandari kuu ya mjini Bujumbura.Muandishi wetu wa Bujumbura, Ramadhani KIBUGA amelizungukia swala hilo na kutuandalia makala haya. Ungana nae
Share





