Raia wa jamuhuri ya kidemokrasia ya congo wanaendelea kumkumbuka, aliyekuwa bondia wa kwanza maarufu mwenyi asili ya Kiafrika, Muhammad Ali, wa Marekani aliyefariki jumamosi iliopita (4Juni2016) akiwa na umri wa miaka 74.
Nizaidi yamiaka arobaini na mbili sasa tangu lilipofanyika pambano la ndondi lililo wakutanisha Mohammed Ali na George forman katika uwanja wa kitaifa TATA RAPHAEL mjini Kinshasa, katiaka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Wakati huo ikijulikana kama ZAIRE. Ni mchezo ambao ulijulikana kama "Rumble in the jungle". Pambano hilo lili ingia katika vitabu vya historia na Mohammad Ali, akawashangaza wengi kwa kuibuka na ushindi dhidi ya Foreman ambaye mpaka wakati huo alikuwa hajawahi kushindwa ulingoni. Ali alifariki katika jiji la Phoenix Arizona, baada ya kulazwa hospitalini.
Mwandishi wetu BYOBE MALENGA alituandalia taarifa ifuatayo kutoka BUKAVU, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo
Share





